WANAUME 18 kati ya waliofika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuhojiwa kuhusu kutelekeza watoto wamekubali kupimwa vinasaba (DNA) na Mkemia Mkuu wa Serikali, taarifa iliyotolewa jana na Paul Makonda ilisema. Continue reading Wanaume 18 Wakubali Kupimwa DNA kwa Makonda
Tag Archives: Paul Makonda
Paul Makonda Akanusha Kuwaita Edward Lowasa, Mbowe
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikiwa na orodha ya majina ya watu akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa na baadhi ya wabunge kuwa wameitwa ofisini kwake kwa madai ya kutekeleza watoto wao. Continue reading Paul Makonda Akanusha Kuwaita Edward Lowasa, Mbowe
Viongozi Wadini na Wabunge wanasa kwa Makonda
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aameweka hadharani kuwa kati ya wanawake 480 waliozungumza na wanasheria siku ya jana Jumatatu katika ofisi za mkoa wamezalishwa na kutelekezwa na wabunge pamoja na viongozi wa dini.
Continue reading Viongozi Wadini na Wabunge wanasa kwa Makonda
“Tutakutangaza hadharani mkeo ajue” – Paul Makonda
Paul Makonda amefunguka na kusema wanaume ambao wamewazalisha wanawake na kuwatelekeza bila kuwapa matunzo pindi watakapoitwa wakikaidi wito huo kwa lengo la kulinda ndoa zao basi watawatangaza hadharani ili wake zao wajue wana watoto nje ya ndoa.
Continue reading “Tutakutangaza hadharani mkeo ajue” – Paul Makonda
MAKONDA ATOA MISAADA KWA WAJAWAZITO WATAKAOJIFUNGUA PASAKA
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda leo ametoa zawadi ya vifaa tiba vya Mama mzazi kwaajili ya kujifungulia (Delivery Packs) 200 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi million 20 Kama zawadi yake ya sikukuu ya pasaka kwa kinamama watakaojifungua kwenye msimu huu wa pasaka. Continue reading MAKONDA ATOA MISAADA KWA WAJAWAZITO WATAKAOJIFUNGUA PASAKA
Viongozi wa Serikali, Wanasiasa watuhumiwa kwa RC
Baadhi ya viongozi wa siasa na viongozi wa serikali wadaiwa kuongoza kutelekeza wanawake waliozaa nao kwa makusudi na kusababisha ongezeko la kinamama kufika kwa mkuu wa mkoa Dar es salaam kuomba msaada wa malezi kwa watoto wao.
Continue reading Viongozi wa Serikali, Wanasiasa watuhumiwa kwa RC
Paul Makonda kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wanaume zao
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewatangazia wawanake wote waliotelekezwa na waume zao na hawapatiwi fedha za matunzo ya mtoto kufika ofisini kwake siku ya Jumatatu ya April 09 kwaajili ya kupatiwa msaada wa kisheria. Continue reading Paul Makonda kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wanaume zao
Ombaomba wakabidhiwa kwa Wakuu wa Mikoa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Selemani Jafo amewataka Wakuu wa Mikoa nchini kubuni mikakati ya kuondoa tatizo la ombaomba mijini.
Paul Makonda awaomba msamaha
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mh. Paul Makonda amefunguka na kuwaomba msamaha baadhi ya wananchi ambao ameshindwa kutimiza ndoto zake na kusema anaamini ataendelea kuwatumikia na kujitahidi kuweza kugusa maisha ya kila mmoja.
MAKONDA AFANIKISHA SAFARI NA MATIBABU YA AHMED ALBAITY CHINA
RC Makonda alitoa ahadi kumsaidia Ahmed Albaity wakati wa Zoezi la Upimaji Afya Bure kwenye Meli ya Jeshi la China mwishoni mwa Mwaka Jana baada ya kugundulika Ahmed anahitaji Matibabu Maalum ambayo hayapatikani kokote kule duniani isipokuwa China, jambo lililomfanya RC Makonda kutokwa na Machozi na Kuhaidi Kumpeleka kwenye matibabu kwa gharama yoyote ile Maumivu na Mateso anayopitia kijana huyo.
Ahmed Albaity anasumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo baada ya kuanguka na kuvunjika Shingo alipokuwa akiogelea ambapo kwa sindano moja pekee inagharimu Dollars 26,000/= sawa na shillingi million 52.
RC Makonda amesema Ahmed atasafiri Nchini China Siku ya Jumapili akiongozana na watu watatu wa kumsaidia kumuhudumia ambapo gharama zake ni zaidi ya Shilingi Million 100.
Aidha RC Makonda amesema Shauku yake ni kugusa maisha ya Mwananchi hata kama ni mmoja atakaekwenda mbele za Mungu na kusema Asante Mungu kwa kutupatia viongozi wetu, ifike mahali tumtumikie Mungu katika nafasi zetu, na katika hilo watu wote watakuwa Sawa na tutawahudumia bila kutarajia chochote kutoka kwao kama sehemu ya utumishi wetu ambapo amewashukuru watu wote waliomchangia na kufanikisha matibabu.
Hata hivyo RC Makonda ametoa wito kwa wananchi wa dini zote kumuombea Ahmed ili aweze kupona na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.
Kwa upande wa Ahmed Albaity amemshukuru RC Makonda kwa moyo wa ukarimu aliouonyesha ambapo ameeleza kuwa ameishi kwa mateso muda mrefu kutokana na kukosa uwezo wa kumudu gharama za matibabu.
Aidha amesema alipokuwa akiomba watu wamchangie wapo waliokuwa wakimvunja moyo kwa kumwambia hawezi kupona lakini RC Makonda ameonyesha moyo wa kipekee.
Continue reading MAKONDA AFANIKISHA SAFARI NA MATIBABU YA AHMED ALBAITY CHINA